Na COSTANTINE MATHIAS, Dodoma.
WIZARA ya Nishati imemhakikishia Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Simiyu, Tina Chenge kuwa itafikisha umeme katika Shule ya Sekondari Bunamhala iliyoko mtaa wa Songambele Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani humo ndani ya siku tano kuanzia leo Juni 8, 2026.
Hayo yamebainishwa leo na Naibu Waziri wa Nishati, Salome Makamba wakati akijibu swali na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Simiyu, Tina Chenge aliyetaka kujua, Ni lini Shule hiyo itapatiwa Umeme ili wanafunzi waweze kusoma katika Mazingira mazuri.
Mbunge huyo ameuliza "Kwa kuwa ni sera. ya serikali kupeleka Umeme kwenye Taasisi za umma, na Kwa kuwa Shule ya Sekondari ya Bunamhala iliyoko mtaa wa Songambele Bariadi, hakuna Umeme, Je ni lini serikali itapeleka Umeme kwenye Shule hii ili wanafunzi waweze kusoma?..."
Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Nishati, Makamba amesema, "Kwanza nimpongeze mama yangu, mama Tina Chenge umekuwa na bidii sana umekuwa ukitushauri kuhakikisha Mkoa wa Simiyu unapata Umeme wa uhakika lakini pia tunafikia Taasisi nyingi za Serikali,"







0 Comments