RAS KAYOMBO AFUNGUA KIKAO KAZI PROGRAMU YA SCALE SIMIYU.

 

Na Mwandishi wetu.

KATIBU Tawala Mkoa wa Simiyu, Prisca Kayombo, amefungua kikao kazi kuhusu utekelezaji wa Programu ya SCALE  ya kukabiliana na  mabadiliko ya Tabia Nchi inayohusu uboreshaji wa mazingira Mkoani Simiyu.

Imeelezwa kuwa Utekelezaji wa Mradi huo unalenga kujenga uwezo kwa jamii ya Mkoa huo kukabiliana na mabadiliko ya Tabia Nchi.

Mafunzo hayo ambayo yaliyofadhiliwa na Benki ya Dunia, na kuratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) yamefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Nyaumata, Wilayani Bariadi.

Akizungumza na Waratibu ngazi ya Mkoa na Halmashauri  waliohudhuria mafunzo hayo, Katibu Tawala Kayombo  amewataka kutekeleza kwa weledi Programu hiyo ili kufikia malengo mahsusi ya Serikali katika kuboresha mazingira.

Amewahakikishia waratibu wa Programu hiyo kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI kuwa Serikali Mkoani Simiyu itashirikiana nao  bega kwa bega kufanikisha  utekelezaji wa  programu hiyo.

Mkoani Simiyu Programu ya Scale inatekelezwa katika Halmashauri mbili ambazo ni Maswa na Meatu ambapo katika ngazi ya Taifa Programu hiyo inatekelezwa katika mikoa 21 na Halmashauri 54 za Tanzania bara.

Mwisho. 





Post a Comment

0 Comments