Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Shinyanga, Mhashamu Liberatus Sangu (kulia), akiweka mshumaa ili kubariki Maji.Akitoa homilia katika Misa ya Mkesha wa Pasaka iliyofanyika katika Parokia ya Mtakatifu Yosefu, Mume wa Bikra Maria, Ndembezi, Manispaa ya Shinyanga, Askofu Sangu amesema waamini wanapaswa kutumia maadhimisho ya Pasaka kama fursa ya kuanza upya maisha yao ya kiroho.
Amewasisitiza kuishi kwa kuakisi matendo mema kwa jamii, wakiongozwa na misingi ya imani na maadili mema.
Aidha, amewaasa kuepuka hasira na matendo maovu, ikiwemo uchochezi, ugomvi na imani za kishirikina, badala yake waongozwe na fadhila za unyenyekevu, utu wema na uvumilivu.
Pia amewakumbusha umuhimu wa kusoma Neno la Mungu mara kwa mara ili kuimarisha imani yao na kuishi kulingana na mafundisho ya Kristo, sambamba na kuwajali wenye uhitaji wakiwemo yatima, wenye huzuni na wafungwa.
Wakati huohuo, Askofu Sangu amewataka wakristo kusherekea sikuu ya Pasaka kwa amani na upendo, wakifuata maadili ya Kikristo
Wakristo duniani kote wameadhimisha Misa ya mkesha wa Pasaka, ambayo ni kumbukumbu ya kufufuka kwa Yesu Kristo, baada ya mateso, kusulubiwa na kifo chake msalabani, na hatimaye kufufuka siku ya tatu.
Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Shinyanga SACP Janeth Magomi (kulia mwenye Miwani) na msaidizi wake akiwa kwenye Misa ya mkesha wa Pasaka Parokia ya Ndembezi
Baadhi ya wasomaji wa Masomo wakisoma masomo kwenye Misa ya Mkesha wa Pasaka katika Parokia ya Ndembezi
0 Comments